Friday, June 22, 2012

Samaki mwenye Sura ya Nyoka



Ama kwa hakika sio wote waishio baharini ni samaki, bwana Whether Brent Crawford amekamata samaki ambao hafahamiki mwenye ana paund 300 na kuvunja historia ya muonekano na kuzua gumzo namna anavyoweza kumudu uzito wake
Bwana  Crawford alikua katika maeneo ya Texas' na alimvua samaki huyo katika ziwa Corpus Christi  ni miongoni mwa watu wachache waliowahi kuvua samaki mwenye uzani mkubwa kama huo
Crawford, ameishi karibu na ziwa hilo kwa takriban muiaka 20  sasa alitaarifiwa na dada mmoja aliyekua akiogelea kwenye ziwa hilo akiwa na vijana wengine watano  ambao ni wadogo kua kuna jisamaki lisilokua la kawaida kwenye ziwa hilo
baada ya ndoano kutupwa ziwani, mtupo mmoja tu akamchoma sehemu ya kichwani jisamaki hilo, mara waya ukajizunguusha mkononi ,ukaanza kumbanda  mvuvi huyo ,na wakati akitahayari, akavutwa mtoni akitanguliza kichwa mtoni .kumbe si mkono tu bali hata mguu wake ulifungwa na mshipi wa kuvulia ,na ndipo mbwa wa mvuvi huyo aitwae Bleux, akaanza kuvuta suruali  yake sehemu ya mguuni na kuzua mvutano wa ajabu kati ya samaki na mbwa huyo mtoni .
lakini baadaye Crawford  alifanikiwa kuupachua mkono wake ,purukushani hiyo ilidumu kwa muda wa dakika 45 anaeleza Crawford, alipoponyoka katika mtego huo aliichukua simu yake ambayo aliiweka kwenye kifuko kisicho ingia maji na kumpigia rafikiye , ambaye alikuja na bastola, na kumvuta samaki huyo kwa kamba na kumkokota hadi nyumbani kwa Crawford.

No comments:

Post a Comment