Wednesday, October 24, 2012

MIRADI YA MAJI: DC AMPA SAA 24 MKUU WA IDARA KUMPA RIPOTI

              Mkuu wa Wilaya ya Magu, Jaqueline Liana akizindua mradi wa maji

            Mkuu wa Wilaya ya Magu, Jaqueline Liana akihakiki kama maji  yanatoka!


                          haya sasa kazi kwenu, maji ndo haya tunakutwisha!

PAMOJA NA HAYO!MKWARA MZITO UMECHIMBWA




Mkuu wa Wilaya ya Magu, Jaqueline Liana amempa saa 24 Mkuu wa Idara ya Maji wa wilaya hiyo kuwasilisha ripoti ya mradi wa maji uliojengwa katika Kijiji cha Bugabu uliofadhiriwa na kampuni ya Alpha Choice ya Mwanza.        

 Amri hiyo ya Liana inatokana na malalamiko ya wananchi wa kijiji cha Bugabu wakati wa uzinduzi wa mradi huo wa maji uliogharimu kiasi cha zaidi ya shilingi million 5.Akizungumza muda mfupi baada ya kuzindua mradi huo wa maji utakaosaidia wananchi wa vijiji vitatu,
Jaqueline Liana amesema kumekuwa na tabia kwa wakuu wa idara na viongozi wa vijiji kutosoma mapato na matumizi ya miradi.Amesema kuwepo kwa usiri katika miradi mbalimbali kunawafanya wananchi kuichukua serikali yao,kitu ambacho kinaweza kuepukwa iwapo suala la kusomwa mapato na matumizi litazingatiwa.

Afisa mtendaji wa kijiji cha Bugabu Rebecca Jonas na baadhi ya wananchi wa kijiji hicho wamezungumzia changamoto mbalimbali kuhusiana na mradi huo wa majiMeneja mauzo wa Kampuni ya Alpha Choice inayomiliki viwanda vya kusindika minofu ya samaki katika nchi za Afrika Mashariki Bruno Mhoja amesema mradi huo wa maji ni makakati wa kampuni kushirikiana na jamii katika miradi ya maendeleo.Mradi huo wa maji ni wa kwanza katika kijiji cha Bugabu kutolewa na wawekezaji ambao utawanufaisha  wananchi zaidi ya laki moja

No comments:

Post a Comment