
Baadhi
ya wakazi wa mjini Singida, wakiwa wamekusanyika katika duka la wakala wa
M-pesa lililopo kwenye taasisi ya elimu ya watu wazima, muda mfupi baada ya
mmiliki wa duka hilo Mashaka Omari Makiya,kujipiga risasi kwa kutumia Bastola
yake na kusababisha kifo chake.