
Senator wa jiji la Nairobinchini Kenya Gideon Mbuvi a.k.a Sonko jana aliitunuku timu ya wanawake ya
mchezo wa volleyball kiasi cha shilingi 300,000 kwa
fedha za Kenya kwa kujituma na akawaahidi kuwaongezea kiasi kama hicho, endapo
watafanikiwa kuwafunga timu kutoka Tunisia leo .
Jana timu hiyo ya Kenya
walifanikiwa kuwafunga timu kutoka Cameroon ukiwa ni ushindi wao wa awali kwa
ushindi wa t 3-0 na hivyo kuendelea kushikilia record yao ya kutofungwa mpaka
sasa katika michuano inayoendelea ya mataifa ya Africa na hivyo kujongea katika
fainali za michezo hiyo kadiri siku zinavyo songa mbele katika kituo cha
kimataifa cha michezo huko Moi vilivyoko katika eneo maarufu la Kasarani.
Mida ya saa kumi na
moja jioni hii inatarajiwa timu hiyo ya
wanawake ya Kenya endapo itaishinda timu kutoka Tunisia! Basi timu itatawazwa kuwa mabingwa
katika nchi za kiafrica.
Sonko wakati
akimkabidhi team manager Ednah Rotich hundi ya fedha hizo 300,000, Senator
Sonko aliwashukuru wachezaji wa mchezo wa volleyball kwa kujitoa naye akawahakikishia
kuwa ataendelea kuwaunga mkono wakanapoiletea sifa nchi yao kupitia kujituma na
kujitoa kwa taifa.
Sonko pia aliahidi
kupeleka sifa ya timu hiyo kwa viongozi wengine nchini humo na kwenda mbele
zaidi kwa makamu wa rais hadi kwa rais Uhuru Kenyatta.
Kenyaimeshashinda
michezo yote mine iliyocheza katika kombe la mataifa ya Africa iliyopigwa
mwishoni mwa wiki iliyopita katika uwanja wa Kasarani ambapo nchi zilizoshiriki ni : Kenya yenyewe , Egypt, Algeria, Cameroon,
Senegal na Tunisia itakayo kipiga leo.
No comments:
Post a Comment