Tuesday, November 5, 2013

TAMKO LA HAKIELIMU KUHUSU UPANGAJI WA VIWANGO VYA ALAMA,MATUMIZI YA ALAMA ENDELEVU ZA MWANAFUNZI NA UFAULU



Ndugu Wahariri,

 Salamu kutoka HakiElimu,


Kufuatia tamko la serikali kuhusu upangaji wa viwango vya alama, matumizi ya alama endelevu za mwanafunzi na ufaulu kwa kidato cha nne na cha sita, HakiElimu imekuwa ikipokea maombi mengi kutoka vyombo mbalimbali vya habari kutaka kujua msimamo wa shirika kuhusu jambo hili  kama wadau wakubwa wa masuala ya elimu.
 
Tafadhali pokea tamko rasmi kutoka HakiElimu kuhusu msimamo wa shirika. Kimsingi uamuzi huu wa serikali  umemshtua kila mtanzania na wengi wanajiuliza tunatengeneza kizazi cha namna gani, hasa katika ulimwengu huu wenye ushindani mkubwa sio tu kwenye soko la ajira; lakini pia maendeleo ya sayansi na tekinologia ambayo pamoja na mambo mengi yanapelekea uhitaji mkubwa wa wataalamu waliobobea kwenye masuala mbalimbali.

Tunaomba tushirkiane kwa pamoja kama watanzania wenye nia ya kuona watoto wetu wakipata elimu bora na si kufaulu tuu mitihani. Mnaweza kutumia tamko hili kwenye magazeti yenu kwa namna mtakavyoona inafaa.

Tunaamini kuwa mtatumia fursa mlizonzao kuelimisha umma wa watanzania kuhusu jambo hili kuwa si la kufurahia kwa kile wazazi wengi wanachodhani kuwa watoto wao watafaulu mtihani; bali kufikiria zaidi kuhusu ujuzi na maarifa waliyopata kwa kipindi walichokuwa darasani na namna wahitimu hawa watakavyoweza kukabiliana na changamoto zilizopo katika ulimwengu wa sasa.

Asanteni sana kwa ushirikiano.


Benedicta Mrema | Media and Advocacy Email: benedicta.mrema@hakielimu.orgMobile Phone: +255 713 068991; Office: +255 22 2151852/3; Fax: +255 22 2152449
Web: www.hakielimu.orgAddress: 739 Mathuradas Street, P.O.Box 79401, Dar es salaam, Tanzania



No comments:

Post a Comment