Showing posts with label ELIMU. Show all posts
Showing posts with label ELIMU. Show all posts

Monday, February 10, 2014

UMOJA WA MATAIFA WASISITIZA UMUHIMU WA KUWA NA UTAMADUNI MZURI WA KUENZI WANAWAKE WANAOLETA MABADILIKO KWENYE JAMII‏





Picha juu na chini ni Mwandishi wa habari na mpiga picha kutoka Ufaransa, Pierre-Yves Ginet akizungumza na wanafunzi wa shule za sekondari mbalimbali za jijini Dar es Salaam na kuwaonyesha picha na kuwapa ufafanuzi wa mambo mbalimbali ambayo wakinamama wamekuwa wakifanya kwa mustakabali kwa kuleta usawa na haki za wanawake duniani.

Friday, February 1, 2013

KATA YA KIPAWA KUZINDUA AWAMU YA PILI YA MRADI WA MAZINGIRA BORA KWA ELIMU BORA



Diwani wa Kata ya Kipawa Manispaa ya Ilala, Bonnah Kaluwa, akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, kuhusu awamu ya pili ya Mradi wa Mazingira Bora kwa Elimu Bora ,utakao zinduliwa kesho katika Kata hiyo. Kushoto ni Meneja wa Mradi huo Regina Ogwai. Mradi huo utafadhiliwa na nchi ya Marekani.

Tuesday, January 8, 2013

WALIOFAULU DARASA LA SABA 2012 KWENDA KAWE UKWAMANI WARIPOTI SHULENI LEO




Mwalimu wa Shule ya Sekondari Kawe Ukwamani, jijini Dar es Salaa, Peter John (wa nne kushoto mwenye suruali) akiwaelekeza baadhi ya wanafunzi walioripoti shuleni hapo leo asubuhi kwa ajili ya kuanza muhula wa masomo ya Sekondari baada ya kufalu mtihani wa darasa la saba wa 2012 na kuchaguliwa kujiunga na shule hiyo. Wanafunzi wote waliochanguliwa kujiunga na masomo ya Sekondari Kidacho cha kwanza, na wale wa sekondari waliokuwa mapumzikoni, wametakiwa kuripoti shuleni hii leo kote nchini.

Tuesday, December 4, 2012

NAFASI ZA UFADHILI WA MASOMO YA SEKONDARI KWA YATIMA WA KIKE.





   NAFASI  ZA  UFADHILI  WA  MASOMO  YA  SSEKONDARI  KWA  YATIMA  WA  KIKE

RafikiElimu  FOUNDATION  ni  Taasisi  isiyokuwa  ya  kiserikali  inayo  jishughulisha  na  Maendeleo  ya  jamii. Taasisi  inapenda  kutangaza  nafasi  za  ufadhili  wa  masomo  ya  sekondari  kwa  waombaji  wenye  sifa  zifuatazo  :
1. Awe    yatima  wa  jinsia  ya  kike  au  awe  masichana  anayeishi  katika  mazingira  magumu.

2.Awe  raia  wa  Tanzania.
3. Awe  anajiandaa  kujiunga  na  masomo  ya  kidato  cha  kwanza  kuanzia  Januari  2013. AU
4. Awe  anajiandaa  kujiunga  na  masomo  ya  kidato  cha  tano   katika  mwaka  wa  masomo 2013/14.
5. Awe   ni  mwanafunzi  ambaye  tayari  anasoma sekondari   lakini   anashindwa/ ama  ameshindwa  kuendelea  na  masomo  yake  kutokana  na  kufiwa  na  wazazi ama  walezi wake.